India: Majiko yaliyoboreshwa yaondolea adha wanawake kuvaa miwani wakipika
MP3•Epizód kép
Manage episode 425393951 series 2027789
A tartalmat a UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations biztosítja. Az összes podcast-tartalmat, beleértve az epizódokat, grafikákat és podcast-leírásokat, közvetlenül a UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations vagy a podcast platform partnere tölti fel és biztosítja. Ha úgy gondolja, hogy valaki az Ön engedélye nélkül használja fel a szerzői joggal védett művét, kövesse az itt leírt folyamatot https://hu.player.fm/legal.
Katikati ya bonde la mto Ganges kaskazini mwa India, ndiko liko jimbo la Bihar ambalo sasa linahaha kutokana na uchafuzi wa hewa, kwani moshi utokao kwenye majiko ya kuni na samadi ya ng’ombe yanasababisha kwa kiasi kikubwa uchafuzi wa hewa. Licha ya maendeleo makubwa ya kutumia gesi kama chanzo cha nishati, halikadhalika nishati itokanayo na samadi, bado familia au kaya maskini zinashindwa kumudu vyanzo hivyo na kujikuta vikutumia kuni au samadi ya ng’ombe kupikia, ambavyo huchafua hewa. Sasa Benki ya Dunia imewezesha kuundwa kwa vikundi vya kujiwezesha au SHGs ambapo wanawake wanapatiwa elimu ya masuala mbali mbali ikiwemo nishati salama na hivyo kuboresha afya zao. Assumpta Massoi kupitia video ya Benki ya Dunia amefuatilia mradi huo na kuandaa makala hii.
…
continue reading
100 epizódok